Maelezo ya jumla
Maambukizi ya virusi vya zika husababisha ugonjwa wa wanadamu unaoitwa maambukizi ya virusi vya zika au homa ya zika.
- Virusi vya zika kwa kawadia vinasambazwa kwenda kwa wanadamu kupitia mbu, hasa mbu aina ya aides. Hata hivyo, virusi vya zika vinaweza pia kusambaa kutoka kwa mtu mmoja mpaka mwingine kupitia majimaji ya mwili, na hii mara nyingi inatokea wakati wa ngono au wakati wa kuongezewa damu.
- Virusi vya zika vinaambukiza sana
- Zamani iliamininaka kuwa maambukizi ya virusi vya zika ni nadra. Lakini takwimu za siku hizi zinaonesha kuwa, wataalamu walikadria vibaya.
- Virusi vya zika vinaaminika kuwa vinasababisha matatizo makubwa kwa watoto wachanga, hasa kwa sababu ya ubongo kushindwa kukua vizuri.
Ni zipi dalili za maambukizi ya virusi vya zika?
Unaweza kuambukizwa virusi vya zika zaidia ya mara moja na unaweza kuonesha dalili mara nyingi. Dalili huanza kuonekana baada ya masaa machache baada ya kuambukizwa virusi vya zika. Inachukua siku kadhaa (kwa kawaida mpaka wiki) kabla ya kuanza kujisikia vizuri. Dalili za virusi vya zika ni pamoja na:
- Homa
- Upele
- Kupoteza hamu ya kula
- Maumivu ya viungo na maumivu ya misuli
- Kutapika
- Kuharisha au kufunga choo
- Maumivu ya mgongo
- Uchovu
- Macho mekundu na maumivu ya macho
- Maumivu ya misuli
Ni nini husababisha maumivu ya misuli?
Virusi vinavyosababisha maambukizi ya virusi hivi huitwa virusi vya zika. Hawa virusi wa zika kwa kawaida vinapatikana katika nchi zinazoendelea na husababisha milipuko baada ya watu kutembelea maeneo yenye virusi hawa. Virusi vya zika kwa kawaida husambazwa na mbu kwenda kwa wanadamu, hasa mbu aina ya Aedes. Hata hivyo maambukizi ya virusi vya zika yanaweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja mpaka mwingine kupitia majimaji ya mwili, na hii inatokea zaidi wakati wa kushiriki ngono au baada ya kuongezewa damu.
Utambuzi
Daktari anaweza kufanya vipimo vya maambara ili kutambua maambukizi ya virusi vya zika. Dalili za virusi vya zika zinafanana na dalili za maambukizi ya virusi wengine, na kufanya utambuzi bila vipimo vya maambara ni ngumu sana.
Uchaguzi wa matibabau
Matibabu bora zaidi ya maambukizi ya virusi vya zika ni kupata mapumziko ya kutosha na kunywa vinywaji vya kutosha. Kama maambukizi ya virusi vya zika yamehisiwa, usitumie dawa bila kuongea na daktari. Muulize daktari kama unahitajika kutumia dawa ili kupunguza homa ya mwili au kupunguza maumivu, baadhi ya dawa zinaweza kukusababishia matatizo. Kwa sababu maambukizi ya virusi vya zika ni maambukizi ya virusi, dawa aina ya antibiotiki hazisaidii. Dawa za kudhibiti virusi (antiviral) hazipendekezwi kwa wagonjwa kwa sababu karibu wogonjwa wote hupona vizuri bila hata kutumia dawa.
Je maambukizi ya virusi vya zika vinaweza kusababisha Guillan – Barre Syndrome
- Kumetambuliwa kuwepo uhusiano kati ya Guillan–Barre Syndrome na maambukizi ya virusi vya zika
- Ni ngumu kutambua kama kimelea fulani anasababisha Guillan–Barre Syndrome
Kuzuia
Hakuna chanjo kwa sasa kutukinga na maambukizi ya virusi vya zika. Wataalam wengi wanafanya kazi usiku na mchana ili kutengeneza chanjo. Kwa sababu ugonjwa unasambazwa na mbu, kutumia njia za kuwadhibiti husaidia sana. Kutumia dawa za kufukuza mbu, kulala chini ya chandarua chenye dawa, kuweka wavu kwenye madirisha, kuvaa nguo zinazokufunika vizuri (suruali na shati ya mikono mirefu). Ukiambukizwa, unaweza tena kuambukizwa baadae. Inashauriwa ktumia dawa ya mbwa baadae.
Kwa wanawake walioambukizwa virusi vya zika wasubiri kwa muda gani kabla ya kupata ujauzito?
Baada ya kuambukizwa virusi vya zika na kupona, hakuna tafiti zozote zinazoonesha kuwa kupata ujauzito unaweza kuleta matatizo.
UNAPASWA KUSUBIRI KWA MDA GANI KABLA YA KUPATA UJAUZITO KATIKA MAENEO YENYE VIRUSI VYA ZIKA |
||
Uwepo wa dalili | Wanawake | Wanaume |
Dalili za zika | Angalau wiki 8 baada ya dalili kuanza | Angalau baada ya miezi 6 aada ya dalili kuanza |
Hakuna dalili za zika | Ongea na daktari kwanza | Ongea na daktari |