Maelezo ya jumla
Kisonono (Gonorrhea) ni ugonjwa wa zinaa.
Je, Nini dalili za kisonono?
Dalili za kisonono huanza kuonekana siku 2 – 5 baada ya kuambukizwa. Hata hivyo, kwa wanaume, dalili zinaweza kuchelewa mpaka mwezi. Watu wengine hawapati dalili kabisa. Wanaweza kuwa hawajui kabisa kwamba wameambukizwa ugonjwa huu, na kwa sababu hiyo hawatafuti matibabu. Hii huongeza uwezekano wa kupata matatizo na hatari ya kuambukiza wengine.
Dalili kwa wanaume ni pamoja na:
- Maumivu wakati wa kukojoa
- Kukojoa mara kwa mara au kushindwa kuzuia mkojo (mgonjwa akibanwa mkojo, ni lazima akakojoe haraka sana)
- Kutoa uchafu kwenye uume (uchafu unaweza kuwa mweupe, njano, au rangi ya kijani)
- Wekundu au kuvimba kwa urethra (huu ni mrija unaobeba mkojo kutoka kwenye kibofu kwenda nje)
- Kuvimba na kuuma kwa korodani
- Maumivu kwenye koo
Dalili kwa wanawake zinaweza kuwa ndogo sana na zisizo maalam, na huenda zikachanganywa na dalili za maambukizi mengine.
Dalili kwa wanawake ni pamoja na:
- Kutoa uchafu ukeni
- Maumivu wakati wa kukojoa
- Kukojoa mara kwa mara/mara nyingi
- Maumivu kwenye koo
- Maumivu wakati wa ngono
- Maumivu makali kwenye sehemu ya chini ya tumbo (kama maambukizi yataenea mpaka kwenye mirija ya uzazi)
- Homa (Kama maambukizi yataenea mpaka kwenye mirija ya uzazi au eneo zima la tumbo)
Kama maambukizi yataenea kwenye damu, homa, kuwashwa, na dalili kama za yabisi kavu zinaweza kutokea.
Kisonono husababishwa na nini?

Kisonono husababishwa na bakteria anayeitwa Neisseria gonorrhoeae. Mtu yeyote anayefanya ngono ya aina yoyote anaweza kuambukizwa kisonono. Maambukizi yanaweza kuenezwa kwa mdomo, uke, uume au mk*ndu. Bakteria huyu hukua kwenye maeneo ya joto na yenye unyevu, hii ni pamoja na mrija unaotoa mkojo mwilini (urethra). Kwa wanawake, bakteria hupatikana kwenye via vya uzazi ( hii hujumuisha mirija ya uzazi, mji wa mimba, na mlango wa mji wa mimba). Bakteria hawa wanaweza kukua hata machoni.
Nani yuko kwenye hatari zaidi kupata kisonono?
Kuna uwezekano mkubwa wa kupata maambukizi ya kisonono kama:
- Una washirika wengi wa ngono
- Una mpenzi mwenye historia ya kupata magonjwa ya zinaa
- Hautumii kondomu wakati wa ngono
- Wewe ni mwanaume unayefanya ngono na mwanaume mwingine
- Unatumia madawa ya kulevya
Utambuzi wa ugonjwa wa kisonono
- Kisonono hutambuliwa baada ya sampuli ya tishu au uchafu unaotoka ukeni/ kwenye uume kutiwa rangi (gram stain) na kisha kuchunguzwa chini ya darubini. Japo njia hii ya utambuzi ni ya haraka, si ya kuaminika sana. Sampuli kwa ajili ya gram stain huchukuliwa:
- Kwenye mlango wa kizazi cha mwanamke
- Uchafu unaotoka kwenye uume wa mwanaume
- Majimaji kutoka kwenye maungio ya mwili-joints
- Culture (sampuli huchukuliwa na kupandwa kwenye sahani maalumu ya maabara, njia hii huwaruhusu bakteria kukua – utambuzi hufanyika kwa urahisi wakikua ), njia hii ni ya kuaminika zaidi. Sampuli kwa ajili ya culture huchukuliwa:
- Kwenye kizazi na mlango wa kizazi cha mwanamke
- Uchafu unaotoka kwenye uume wa mwanaume
- Kooni kwa wanaume na wanawake
- Mk*nduni kwa wanaume na wanawake
- Majimaji kutoka kwenye maungio ya mwili- joints
- Damu
Matokeo ya awali ya culture hutoka baada ya masaa 24 na matokeo thabiti ndani ya masaa 72.
Wakati gani utafute matibabu ya haraka?
Kama una dalili za kisonono unapaswa kumwona daktari mapema iwezekanavyo.
Uchaguzi wa matibabu ya kisonono
Kuna malengo mawili katika kutibu magonjwa ya zinaa, hasa ambayo yanaenea kwa urahisi kama kisonono. La kwanza ni kutibu maambukizi ya mgonjwa. La pili ni kuwatafuta na kuwapima watu wengine wote ambao wamefanya ngono na mgonjwa, ili kuwatibu na kuzuia maambukizi zaidi. Usijitibu mwenyewe bila kuonwa na daktari kwanza. Mtoa huduma wa afya ataamua ni matibabu gani yaliyo bora zaidi. Matibabu yanayopendekezwa ni pamoja na:
- Sindano moja ya ceftriaxone 125 mg au kumeza dozi moja ya cefixime 400mg.
- Dozi moja ya Azithromycin 2g inaweza kutumika kwa watu wenye mzio kwa ceftriaxone, cefixime, au penicillin.
Mgonjwa anapaswa kurejea hospitalini baada ya siku 7. Vipimo vitafanywa tena, kuhakikisha maambukizi yamekwisha. Watu wote waliofanya ngono na mgonjwa wanapaswa kutafutwa ili wapimwe na kutibiwa. Hii hupunguza kuenea kwa kisonono.
Nini cha kutarajia ukiwa na kisonono?
Kwa karibu mara zote, maambukizi ya kisonono ambayo hayajaenea kwenye damu au maeneo mengine hupona vyema baada ya kutumia antibiotiki. Kisonono ambayo imeenea ni tatizo kubwa, lakini pia hupona baada ya matibabu.
Matatizo yanayoweza kutokea ukiwa na kisonono
Matatizo yanayoweza kutokea kwa wanawake ni pamoja:
- Kuharibika kwa mirija ya uzazi (salpingitis ) – hii inaweza kusababisha ashindwe kupata mimba au kusababisha mimba itungwe nje ya mji wa mimba (ectopic pregnancy).
- Ugumba (kukosa uwezo wa kuwa mjamzito)
- Maumivu wakati wa ngono
- Wanawake wajawazito wenye kisonono wanaweza kuwaambukiza watoto wao wakiwa tumboni au wakati wa kuzaliwa
Matatizo kwa wanaume ni pamoja na:
- Mgonjwa anaweza kupata makovu yanayoweza kusababisha kuziba kwa njia ya mkojo (urethra)- hii inaweza kusababisha shida wakati wa kukojoa
- Jipu (usaha kwenye urethra)
- Matatizo wakati wa kukojoa
- Maambukizi kwenye njia ya mkojo
- Kushindwa kwa figo kufanya kazi
Matatizo yanayoweza kuwapata wanaume na wanawake ni pamoja na:
- Kusambaa kwa maambukizi mwili mzima- hii inaweza kuwa hatari sana
- Kama mgonjwa hatatibiwa mapema, anaweza kuwa na maumivu ya muda mrefu ya maungio (joints).
- Maambukizo ya vali za moyo
- Kuvimba kwa tando za uti wa mgongo au ubongo
MAELEZO ZAIDI KUHUSU UGONJWA WA KISONONO
Maelezo ya jumla
Ni ugonjwa unaosababisha kutokwa usaha kwenye via vya uzazi
Sababu
Neisseria gonorrhea
Epidemiolojia
Unapatikana dunia nzima, unaathiri jinsi zote mbili, hasa vijna na watu wazima wanaojihusisha na ngono kwa wingo. Inawapata zaidi watu wenye uchumi duni. Katika nchi nyingi zilizoendelea kiwango cha maambukizi kimepungua katika miongo hii miwili iliyopita
Uambukizo
Kwa kushiriki ngono na mtu aliyeambukizwa
Muda kabla dalili kuanza
Siku 2-7
Muda wa uambukizo
Mtu anaweza kuendelea kuambukiza wengine kwa miezi mingi kama asipotibiwa. Matibabu ya uhakika yananamaliza uwezo wa kuambukiza baada ya masaa tu.
Nani yuko kwenye hatari
Mtu yeyote anaweza kuambukizwa. Hakuna mtu anayepata kinga na mtu anaweza kuambukizwa mara nyingi sana kisonono
Dalili
- Wanaume
-
- Unahusisha njia ya kutoa mkojo (urethra)
- Kutoa uchafu kama usaha kwenye uume, maumivu wakati wa kukojoa na kukojoa mara kwa amra
- Wanawake
-
- Wanawake wengi hawapati dalili.
- Wanaweza kutokwa na majimaji ukeni.
- Sehemu inayoathiriwa na kisonono mara nyingi ni mlango wa kizazi, mkundu na koo.
- Tezi iliyoko ukeni inayoitwa Bartholin inaweza kuvimba.
- Kuvimba kwa mirija ya uzazi kunatokea kwa 20% wanawake
- Watoto waliozaliwa na kina mama walioambukizwa hutoa usaha kwenye macho, kuwa mekundu na kuvimba kwa siku 2-3
Utambuzi
- Kuangalia kwa darubini sampuli kutoka ukeni, mrija wa kojo, mlango wa kizazi, kope za macho – gram stain
- Culture
Matibabu
- Co – trimoxazole AU
- Erythromycin AU
- Ceftriaxone
Kuzuia
- Toa matibabu kwa wagonjwa
- Tibu wapenzi wa wagonjwa pia
- Toa elimu kuhusu ngono salama
- Dhibiti magonjwa ya ngono kwa wanaouza milii (Malaya)
-
- Vipimo vya kila mwezi na kutoa matibabu
- Kuwagawia kondomu
- Kuchunguza wanawake wajawazito na kutoa matibabu mapema ili kuzuia kuambukiza mtoto
- Kupaka dawa aina 1% tetracycline kwenye macho ya mtoto baada tu ya kuzaliwa
asante kwa makala hii watalaamu
Karibu
Je kisonono kinaweza kusabababisha mchubuko mwekundu juu ya kichwa cha uume
hAPANA, Kisonono haisababishi vidonda, kisonono inasababishwa kutoka na uchafu ukeni au kwenye uume , uchafu unakuwa mzito, wa njano kama usaha
Karibu sana
Kisonono linaweza sababisha mowasho ukeni?
Ndio unaweza kuwashwa ukeni, mwasho kama unaungua hasa unapokojoa. inaweza kuambatana na kutokwa uchafu mzito kama usaha . Mwone dakatari akuandikie dawa
Kisonono kinaweza sababisha miwasho ukeni?
Ndio unaweza kuwashwa ukeni, mwasho kama unaungua hasa unapokojoa. inaweza kuambatana na kutokwa uchafu mzito kama usaha . Mwone dakatari akuandikie dawa
Je Kwa mwanamkee Kuwa na dalili moja kati ya hayo ni dalili za kisonono? mfano kutokwaa na uchafu ukeni.
Dr kitu gani kinachofanya uume kua na vidonda vinavyowasha sana unajikuna hadi kuchubuka sana