Maelezo ya jumla
Kuwashwa (itching) ni hali ya kuhisi mchonyoto unaokera kwenye ngozi anaokufanya utamani kukuna sehemu ilioathiriwa. Unaweza kuwashwa sehemu fulani ya mwili pekee au mwili mzima.
Kuwashwa husababishwa na nini?
Kuna sababu nyingi za kuwashwa, ikiwa ni pamoja na:
- Kuzeeka kwa ngozi
- Kuvimba kwa ngozi kunakosababishwa na mzio –atopic dermatitis
- Kuvimba kwa ngozi kunakosababishwa na kugusa vitu vinavyosumbua na kuwasha ngozi (Kugusa sumu ya mti wa mwaloni au mwefeu)-contact dermatitis
- Kugusa vitu vinavyoudhi au kuunguza ngozi (kama vile sabuni, kemikali, au pamba)
- Ngozi kavu
- Ugonjwa wa mabaka ngozini- hives
- Kuumwa na wadudu
- Vimelea kama vile minyoo, chawa wa mwili, chawa wa kichwa, au chawa wa mavuzi
- Magonjwa ya ngozi kama pityriasis rosea au psoriasis
- Upele
- Kuunguzwa na mwanga wa jua
- Maambukizi ya ngozi kama vile kuvimba kwa vinyweleo (folliculitis) au maambukizi yanayosababisha malengelenge (impetigo)
Kuwashwa mwili mzima kunaweza kusababishwa na:
- Athari inayotokana na mzio (allergic reaction)
- Maambukizi ya utotoni (kama vile tetekuwanga (chickenpox) au surua (measles))
- Homa ya manjano (inayoashiriwa na ini kuvimba)- hepatitis
- Upungufu wa damu (anemia) unaosababishwa na upungufu wa madini ya chuma mwilini
- Ugonjwa wa figo
- Ugonjwa wa ini unaosababisha manjano
- Ujauzito
- Matokeo mabaya ya dawa na vitu kama vile antibiotiki (penicillin, sulfonamides), dhahabu, griseofulvin, isoniazid, opiates, phenothiazines, au vitamini A
Utambuzi
Daktari au muuguzi atakuchunguza na kuuliza maswali kadhaa kuhusu historia yako ya kimatibabu na dalili.
Unaweza kuulizwa maswali yafuatayo:
- Umekuwa ukiwashwa kwa muda gani sasa?
- Je! Unawashwa muda wote?
- Je, kwuwashwa kunaongezeka makali au kuenea?
- We unadhani ni nini kinasababisha unawashwa?
- Je! Umeshawahi kuwashwa kwa namna hii huko nyuma? Ni nini kilichosababisha uwashwe kipindi hicho?
- Je! Umekutana na kitu chochote kinachoweza kusababisha kuwashwa ngozi hivi karibuni?
- Je! Una mzio na kitu chochote au uko-sensitive na kitu fulani?
- Je, unatumia dawa gani?
- Je! Umeanza kutumia bidhaa yoyote mpya hivi karibuni? Ni ipi?
- Je! Umetumia sabuni mpya, kitambaa , marashi, manukato, au kemikali?
- Je! Ulikuwa karibu na wanyama?
- Je, umekula samakigamba (shellfish) au njugu/karanga hivi karibuni?
- Je! Umeumwa na mdudu/wadudu hivi karibuni?
- Je, unapaka losheni kwenye ngozi yako?
- Je, umekaa kwa muda mrefu juani hivi karibuni?
- Je! Unawashwa sehemu gani ya mwili wako?
- Je, Unawashwa mwili mzima?
- Je, unawashwa eneo gani la mwili? Ni eneo lipi?
- Je! Sehemu ya ngozi inayowasha inaonekanaje?
- Je, kuna upele? Ikiwa ndivyo, je, kuna malengelenge, magamba au ukurutu?
- Je, unatibiwa ugonjwa au hali nyingine yoyote?
- Je, Una dalili nyingine zozote?
Wakati gani utafute matibabu ya haraka?
Mwone daktari au muuguzi kama unawashwa na:
- Una dalili nyingine zisizoeleweka
- Makali ya muwasho yanaongezeka
- Muwasho hauishi
- Hakuna sababu ya dhahiri ya kuwepo huo muwasho
Mara nyingi mgonjwa anaweza kutathmini na kutambua ni nini kinachosababisha muwasho bila msaada wa daktari. Jaribu kutafuta sababu inayoweza kusababisha muwasho ukiwa nyumbani.
Wakati mwingine ni rahisi sana kwa mzazi kugundua sababu ya kuwashwa mtoto. Kuangalia kwa karibu ngozi kutakusaidia kutambua kama umeumwa na mdudu, upele, ukavu wa ngozi, au ukurutu. Mara nyingi sababu ya kuwashwa iko wazi na dhahiri, kama vile kuumwa na mbu.
Hakikisha unamwona daktari mapema iwezekanavyo kwa uchunguzi, kama haujui sababu ya muwasho na unarudi mara kwa mara , kama unawashwa mwili mzima ,au una mabaka mwilini kila mara. Kuwashwa mwili kusiko na sababu inayojulikana kunaweza kuwa dalili ya ugonjwa hatari.
Uchaguzi wa matibabu kwa tatizo la kuwashwa
Kama muwasho ni mkali sana au unadumu kwa muda mrefu, ni muhimu kuonana na mtoa huduma wa afya kwa ajili ya utambuzi na matibabu.
Wakati huo huo, unaweza kuchukua hatua kadhaa ili kusaidia kukabiliana na muwasho:
- Epuka kukuna au kusugua eneo linalowasha.
- Hakikisha kucha zako ni fupi ili kuepuka kuchuna ngozi unapojikuna.
- Vaa nguo za kuzuia baridi au mwanga, na vaa nguo zisizobana unapolala
- Epuka kuvaa nguo zinazokwaruza kwaruza, hasa pamba, katika eneo lenye muwasho.
- Oga kwa kutumia maji ya vuguvugu na sabuni kidogo.
- Jipake losheni kulainisha na kupunguza ukavu wa ngozi
- Ukavu wa ngozi ni chanzo kikubwa cha muwasho
- Kama eneo linawasha sana unaweza kuweka kitambaa chenye barafu au ubaridi.
- Epuka kukaa sana karibu na moto au joto kali.
- Fanya shughuli nyingi mchana ili usiufikirie muwasho na kukuchosha sana ili ulale vizuri usiku
- Unaweza kujaribu kutumia dawa zinazouzwa duka la dawa kama vile antihistamines mfano diphenhydramine, lakini uwe makini na madhara yanayoweza kutokana na dawa mfano usingizi.
- Jaribu cream ya hydrocortisone kwenye sehemu zinazowasha .
Mm nina mwasho kichwani kwwnye kisogo, kwenye utosi hapo nywele zinapoanzia kwenye kidevu na kwenye pua pia kiunoni nizaidi ya mwaka sasa vjui nitumie dawa gani.nikijikuna vinatoka vpele vidogo vidogo vinatoa majmaji ambayo baada ua mda yanakauka kama utomvu fulani kama mchanga naombeni ushauri wenu
Habari Samson
Nimejaribu kuelewa Swali lako lakini nimeshindwa, kwa hiyo sitaweza kukupatia jibu
Tafadhali kama utaweza, tuandikie tena kwa kirefu jinsi unavyogonjeka
■Itapendeza kama utauliza swali kupitia ukurasa wetu wa mijadala ili tulijadili swala lako kwa pamoja na wataalamu wengine
Kila napomaliza kuoga uwa na washwa mwili mzima ningependa fahamu inatokana na nini…?
Pole sana
Kwanza inabidi kujiangalia kama unavimba baada ya kuoga, kuna baadhi ya bidhaa za kuogea zinaweza kusababisha mzio kwa baadhi ya watu, kama ukiogea aina fulani ya sabuni na mwasho ukazidi basi badili
Sababu kubwa ya tatizo hili ni ukavu wa ngozi, ngozi inapokuwa imekauka sana hasa baada ya kuoga, inawasha
Ukioga maji ya moto na kutumia sabuni, unaondoa mafuta mengi kwenye ngozi na kuiacha ikiwa kavu kabisa, kwa watu ambao ngozi yao ni senstive wanawashwa
Mambo ya kufanya
■ Usijifute maji kwa taulo unapojikausha, ni vizuri kuji peti peti badala ya kujifuta ili unyevu ubakie kwenye ngozi
■ Paka mafuta, lotion au moisturizer mara tu baada ya kuoga ili kuufungia huo unyevunyevu ndani ya ngozi yako
■ Epuka kuoga maji ya moto kama unaweza, maji ya ngizi yanaondoa kwa kiasi kikubwa mafuta kwenye ngozi na kuiacha ikiwa kavu sana
Asante na karibu tena
Nawashwaa usoniii nikiwaaa panavimbaa na sehem mbalimbali ya mwilii zaman sikuawah washwaa kabisaa na sijuii tatizoo nn mpakaa sasa
Ooh pole sana , mara nyingi mwasho wa aina hiyo ambao haukuwepo zamani, unatokana na mzio kwa kitu kipya ulichoanza kutumia
Angalia kama kuna kipodozi kipya ulichoanza kutumia au ondoa vipodozi vyote na mafuta anza kutumia kimoja kimoja ili uone ni kipi kinaleta shida
Kuna Kaka angu muda wote anashinda anajikuna tu mwili mzima inaonesha Kama una ukurutu kutokana na kujikuna tumeshindwa kujua chanzo Ni Nini na tatizo litatibika vipi
Naomba msaada wako Dr
Habar Dr mi nawashwa najikuna sana mpaka vipere vinatokea usoni,kidevu,kiuno,kwenye vidole vya mkono mguuni mpaka kidonda kinatokea tena huwa nawashwa haswa saa 12jion mpaka ntakapo lala naomba msaada wKo
mimi nawashwa mwili mzima navimba kama vinundunundu tatizo lina mda mrefu
Naomba unisaidie kujua tatizo na suluhisho la mtu anaetokwa na makovu baada ya kuugua kaupele na badae kukakuna na kakaleteleza kovu mwilini hiyo inasababishwa na nn na huyo mtu anaweza akatumia dawa gani kuondokana na hilo tatizo
Samahani mimi napatwa shida sana ya kuwashwa hasa usiku mida nikitaka kulala sehemu za mapaja nmejaribu kutumia aina kidogo lakin kilakuwa kinapoza vmeisha muwasho bado upo palepale na hasa mda wa usiku nikitaka kulala tu sehemu za mapaja na muwasho wale ni ule nikijukuna natamani zaid kujikuna naomba msaada kujua shida ni nini
kama ukiweza, naomba uniandikie katika namba iliyopo hapo chini, ili tuzungumze vizuri na kwa kirefu ili kutafuta sababu ni nini?
Mimi nawashwa pindi tu jua linaponichoma na pia nikipata msisimko tatizo ni nini?
Mimi nawasha tuu mwili lakini sioni chochote
Polee,ni vizuri kuonana na daktari achukue maelezo na vipimo akusaidie. pole sana
Kujamiana kunaweza kupelekea muwasho wa mwili au nimehisi vibaya
Mimi nawashwa sehem za Siri nahisi Kuna wadudu doctor kabisa wadudu wapo nimejaribu kunyoa zoote lakin bado muwasho upo palepale sijui tatizo nini
Pole sana, zipo sababu nyingi sana za mwasho sehemu za siri. ni vizuri kumwona daktari aangalie tatizo ni nini akusaidie. Usiendelee kuvumilia
Na sumburiwa na ttzo lakuwashwa. Na ngozi nimejaribu kutmia dawa lkin naona bado
Ili kutibu mwasho ni vizuri kutambua kwanza sababu ni nini?
kama unashindwa kutambua ni vizuri ukaongea na daktari
Doc mim nawshwa kam week ya 3 natmiaa dawa nkiaacha vinarudi nmeend hsptl napew dawa lakn nado na nkijikuna oanafnya kam vipele yaan uvimbe af nakua mwekundu jaman msaaada nimechoka na hii hali
Nina wiki 3 nawashwa mwili kwa kuruka ruka maeneo ya mwili,hasa nikiwa sehemu yenye joto naomba msaada
Ongea na daktari wetu, kupitia nmba iliyopo kwenye tovuti, utahitajika kutoa maelezo zaidi
Tatizo lako kama langu na kwa watu wengi pia limewakuta hili, kama mm na mwanangu wote tunajikuna balaa hasa usiku
Pole sana, kama ulivyosoma katika makala hii, kuwashwa kunasababu nyingi, na daktari anahitaji kuuliza maswali ya mwongozo kwa mgonjwa ili kutambua sababu ni nini kabla ya kutoa tiba. ni vyema kuongea na daktari wetu ili kupata ushauri unaokufaa wewe, ili kupta nafuuu. pole sana kwako na familia yako
Kujikuna kila mda mtoto wa miaka 3 tatizo ni nini
Sababu zinaweza kuwa nyingi, kama umesomaakala hii unaweza kuwa na idea ni nini sababu
Jaribu kushughulika na mambo ya kawaida yanayoweza kusababisha tatizo, ikishindikana mwone daktari
Kama yuko kwenye jua mtoe hapo, kama kuna nyasi mtoe hapo, kama amevaa nguo mpya mbadilishie, kama umeenda ugenini kagua malazi anayolalia yanawza kuwa na wadudu, kama kuna upepo mkali mpake mafuta mwilini au jifukize kwa maji ili kuweka unyevu kwenye ngozi
Unaweza pia kununua dawa za kupooza mwasho kama cetrizine au dawa za kupaka, ila ni vzr kutafuta sababu ni nin
Hua ninawashwa nyayo ya mguu wa kushoto nimiaka mi2 sasa sijui chanzo ni nini naomba msaada au ushauli
Naomba number yako ya simu nikupigie ili nikueleze tatizo langu
0759078960