Maelezo ya jumla
Maumivu ya tumbo ni maumivu yanayotokea popote kati ya kifua na kinena.
Dalili za maumivu ya tumbo?
Karibu kila mtu hupata maumivu ya tumbo kwa wakati mmoja au mwingine, na mara nyingi maumivu haya hayasababiswi na ugonjwa mkubwa. Ukali wa maumivu ya tumbo hauashirii kuwa ugonjwa wako ni mkubwa au la.
Kwa mfano, unaweza kuhisi maumivu makali sana ya tumbo ukiwa na gesi tu tumboni au maumivu ya tumbo yanayosababishwa na kuvimba kwa utando-ute wa tumbo unaosababishwa na virusi.
Kwa upande mwingine, hali zinazoweza kutishia maisha kama vile saratani ya utumbo mpana au kibole zinaweza kusababisha maumivu ya kawaida tu au yasiwepo kabisa.
Njia nyingine za kuelezea maumivu ya tumbo ni pamoja na:
- Maumivu yanaweza kuwa kwenye tumbo lote. Hii ni kawaida kwa mtu aliyevimbiwa au mwenye gesi tumboni. Maumivu yanaweza kuwa makali sana baada ya kuziba kwa utumbo.
- Maumivu ambayo yako kwenye sehemu maalumu huashiria kuwa kuna tatizo katika kiungo kimojawapo tumboni, kama vile kidole tumbo, mfuko wa nyongo, au tumbo.
- Maumivu na tumbo kubana si tatizo kubwa, na mara nyingi husababishwa na kuvimbiwa ambako mara nyingi hufuatiwa na kuhara. Ishara zinazoonesha kuwa hali ni mbaya ni pamoja na maumivu yanayotokea mara kwa mara, yanayokuwepo kwa zaidi ya masaa 24, na kutokea kwa homa.
- Maumivu menine huja na kuondoka. Maumvu haya huanza na kukatika ghafla, na mara nyingi ni makali sana.Mara nyingi aina hii ya maumivu husababishwa na mawe kwenye figo au mfuko wa nyongo.
Ni nini husababisha maumivu ya tumbo?
Hali nyingi zinaweza kusababisha maumivu ya tumbo. Kitu muhimu ni kujua ni wakati gani unahitaji kupata huduma za matibabu ya haraka.
Sababu za maumivu kwenye tumbo ni pamoja na:
- Kufunga choo
- Mzio wa chakula (kama vile mzio wa bidhaa za maziwa)
- Kula chakula kichafu
Sababu nyingine ni pamoja na:
- Kibole
- Kuziba kwa utumbo au tumbo
- Saratani ya tumbo, koloni, na viungo vingine
- Kuvimba kwa mfuko wa nyongo au mawe kwenye mfuko wa nyongo
- Kupungua kwa mtiririko wa damu kwenye tumbo au utumbo
- Kiungulia, kuvimbiwa, au Kucheua
- Ugonjwa wa kuvimba utando ute wa tumboMatumbo ya uchochezi (Crohn’s disease au ulcerative colitis)
- Mawe kwenye figo
- Kuvimba kwa kongosho
- Vidonda vya tumbo
Wakati mwingine maumivu ya tumbo yanaweza kusababishwa na tatizo mahali pengine mwilini, kama vile kifuani au eneo la nyonga. Kwa mfano, unaweza kuwa na maumivu ya tumbo kama una:
- Mshtuko wa moyo
- Kukaza kwa misuli
- Ugonjwa wa kuvimba kwa mirija ya kizazi na kizazi (PID)
- Nyumonia
- Maumivu makali yanayosababishwa na hedhi
- Mimba iliyotungwa nje ya mji wa mimba
- Maambukizi kwenye njia ya mkojo
Utambuzi wa maumivu ya tumbo
Mtoa huduma ya afya atafanya uchunguzi wa mwili na kuuliza maswali kuhusu dalili zako na historia ya tatizo lako. Ukali wa dalili, mahali maumivu yalipo na muda yanapotokea. Majibu ya maswali haya na mengine mengi yatamsaidia daktari kufanya utambuzi.
Unaweza kuulizwa maswali yafuatayo:
- Unahisi wapi maumivu?
- Je, maumivu yametapakaa kwenye tumbo lote au mahali fulani maalumu?
- Je, maumivu yanatapakaa kwenda kwenye mgongo, kinena, au miguu?
- Je, maumivu ni mkali sana, yanakata, au kubana?
- Je, unapata maumivu wakati wote au yanakuja na kuondoka ?
- Je, maumivu yanakuamsha usiku toka usingizini?
- Je, umewahi kupata maumivu kama hayo hapo zamani? Yalidumu kwa muda gani?
- Je! Maumivu hutokea wakati gani? Kwa mfano, kabla ya kula, baada ya kula au wakati wa hedhi?
- Ni nini husababisha maumivu kuwa makali zaidi? Kwa mfano, kula, msongo, au kulala chali?
- Ni nini hufanya maumivu kupungua? Kwa mfano, kunywa maziwa,na kula chakula?
- Je! maumivu hupungua baada ya Kuharisha, au kutumia dawa za kupunguza asidi tumboni?
- Je, unatumia dawa gani?
- Umekuwa na jeraha la hivi karibuni?
- Je! Una ujauzito?
- Una dalili gani nyingine?
Vipimo vinavyoweza kufanyika ni pamoja na:
- Barium enema
- Vipimo vya damu, mkojo, na kinyesi
- Colonoscopy au sigmoidoscopy
- CT scan
- EKG (electrocardiogram)
- Ultrasound ya tumbo
- Eksirei ya tumbo
Ukiwa na maumivu ya tumbo ni wakati gani utafute matibabu ya haraka?
Tafuta usaidizi wa haraka kama:
- Uko kwenye matibabu ya saratani
- Una mimba au kuna uwezekano ukawa mjamzito
- Hupati kinyesi, hasa ikiwa unatapika pia
- Unatapika damu au kuna damu kwenye kinyesi chako (hasa ikiwa ni cheusi au chenye rangi kama lami)
- Umepata jeraha tumboni hivi karibuni
- Una maumivu kifuani, shingoni, au kwenye mabega
- Unapata shida kupumua
- Una maumivuma ndani, au katikati ya bega yako na kichefuchefu
- Umepata maumivu makali ya tumbo ghafla
- Tumbo lako linauma likiguswa au limekuwa gumu na lililokakamaa sana
Mwone daktari kama una:
- Usumbufu tumboni unaodumu kwa wiki 1 au zaidi
- Maumivu ya tumbo ambayo hayapoi baada ya masaa 24 – 48, au yanakuwa makali zaidi, yanatokea mara kwa mara na una kichefuchefu na kutapika
- Kuvimbiwa kunakodumu kwa zaidi ya siku 2
- Maumivu wakati wa kukojoa au unakojoa mara kwa mara kuliko ilivyo kawaida, hasa usiku
- Kuharisha kwa zaidi ya siku 5
- Homa (zaidi ya 100 ° F kwa watu wazima au 100.4 ° F kwa watoto)
- Kukosa hamu ya chakula kwa muda mrefu
- Kutokwa damu ukeni kwa muda mrefu
- Kupungua kwa uzito bila sababu maalumu
Uchaguzi wa matibabu ukiwa na maumivu ya tumbo
Kama una maumivu ya tumbo ya kawaida tu, vidokezo vifuatavyo vinaweza kusaidia:
- Kunywa maji kidogo au kinywaji kingine chepesi.
- Epuka kula chakula kigumu kwa masaa kadhaa ya mwanzo.
- Kama unatapika, subiri masaa 6, kisha kula kiasi kidogo cha chakula chepesi kama vile wali, ndizi, au uji. Bidhaa za maziwa zinapaswa kuepukwa.
- Maumivu yakiwa kwenye sehemu ya juu ya tumbo na yakiwa yanatokea baada ya kula chakula, antacids zinaweza kusaidia, hasa kama unapata kiungulia au umevimbiwa . Epuka kula vitu vichachu , yakula vyenye mafuta mengi, bidhaa za nyanya, kahawa, na vinywaji baridi.
- Epuka kutumia aspirini, ibuprofen au dawa nyingine za kupunguza uvimbe au maumivu kama haujaagizwa na daktari.
Dawa za kuepuka
Wagonjwa wanaopata maumivu ya tumbo bila kuharisha wanapaswa kuepuka kutumia dawa zifuatazo:
- Loperamide
Kama unapata maumivu ya tumbo bila kuharisha, ongea na daktari kabla ya kuanza au kuacha kutumia moja ya dawa hizi.
Kuzuia
Hatua zifuatazo zinaweza kusaidia kuzuia aina fulani za maumivu ya tumbo:
- Epuka kula vyakula vyenye mafuta mengi .
- Kunywa maji ya kutsha kila siku.
- Kula chakula kidogo kidogo mara kwa mara.
- Fanya mazoezi mara kwa mara.
- Punguza kula vyakula vinavyozalisha gesi.
- Hakikisha kwamba unakula mlo kamili. Kula matunda na mboga kwa wingi.
Nina maumivu ya tumbo na sijajua Nini cha kufanya
Pole sana Mr.Sigera, kwa bahati mbaya haujatuambia maumivu yako yalianza lini?, unaharisha? unatapika? una homa? kuna kitu umekula ambacho kinaweza kusababisha? una historia ya vidonda vya tumbo. Kwa sababu maumivu ya tumbo ni dalili kama dalili nyingine, ni ngumu kujua tatizo lako kama hatuna taarifa za nyongeza. Kama maumivu ni makali sana, nashauri ufike kituo cha afya. unaweza kutumia dawa za maumivu ili kupunguza karaha. kama una ”ibuprofen” au ‘acetaminophen”tumia hizo. kisha mwone daktari. Pole sana.
Habari
Mimi nilikuwa mjamzito lkn kwa bahat mbaya uliharibika trh30 mwezi wa 8 nikasafishwa na nikawa sawa kabisa badae sasa mwezi wa10 nikashika ujauzito mwengine nabaada yakufikisha week4 nikaanza kupata maumivu tumboni chini yakitovu kuzunguka kote kwenye kiuno naenda hospital napimwa napewa dawa nazitumia mara nkaanzwa kutokwa namaji maji mepesii nikarudi hospital nikafanyiwa ultrasound nikapewa maelekezo pamoja na dawa kweli maji yakakata siku 2 tena nikaanza kuona bld ila kidogo kidogo na maumivu makali na matatizo yote haya hunitokea wakati wausiku mchana nakuwa poa kabisa yanii…cha kushangaza kabisa leo nimepima mwenyew kipimo kinaonyesha sina ujauzito…naomba unisaidie kwa hili tafadhali
Pole sana. Ila kwa bahati mbaya kwa sasa siwezi kukusaidia, ni vizuri kumwona daktari moja kwa moja akupime na kukufanyia uchunguzi ajue tatizo ni nini?. Pole sana
ninashida ya tumbo kubana mara ya kwanza ilinitokea mwaka jana mwezi wa kwanza nkaenda hospital nkakutwa na alcers nkatumia dawa baada ya muda nkaka sawa lkn hali hiyo imenirudia tena hasa kipindi nikiwa cjala kitu sasa cjajua tatizo litakuwa ni alcers au kuna kingine cha zaidi
Vidonda vya tumbo ni tatizo linaloweza kutibiwa vizuri a likapona. lakini pia linaweza kujirudia kama mamabo yaliyosababisha vidonda hapo awali hayatondolewa. Vidonda vya tumbo ni kama vidonda vingine, hata kama utatibiwa na kupona kama kilichokuumiza hakitaondolewa utapata kidonda tena
Ninakushauri usome makala yetu inayozungumzia vodonda vya tumbo ili kujifunza zaidi. kama bado utakuwa na maswali tuulize tutakujibu, ASANTE BONYEZA HAPA
ninashida ya tumbo na cjaenda period 3months cna usiano wa kimapenzi
Pole sana
Hii shida ya tumbo haujaieleza vizuri kwa hyo siwezi kuijibia
Ila hili la kukosa hedhi miezi 3 linaweza kutokea kwa sababu nyingi
Unaweza kukosa hedhi kwa sababu ya mabadiliko ya ki mazingira, kwa sababu ya msongo wa mawazo , kwa sababu ya kufanya shughuli au mazoezi magumu
Unaweza kukosa hedhi pia kama umepata ujauzito, una maambukizi makali ya mfumo wa uzazi na nyingine nyiiingi
Kama.una wasiwasi ninashauri , ufike na kumwona daktari, atachukua historia na kukufanyia uchunguzi na ikibidi vipimo atambue sababu ni ipi na kukupatia matibabu stahiki
Pole sana na karibu
Nina maumivu ya tumbo ya kuja na kuondoka…. Ila pia inambatana na maumivu ya shingo,mabega na pia viungo vya mwili
ni vzi kumwona daktari atambue sababu ni nini
Daktari najua. Ni mada ya tumbo lakin naamini unaweza kunisaidia hili mm kilkilasiku napiga mswaki lakin nashindwa kuelewa yakua sijuii kinywa ni kichafu au ni damu ndouwa zinanitoka ni kilasiku inatokea unaweza nosaidia hata ushauri
pole sana
kupiga mswaki ni swala la msingi, na la kila siku
Ni vizuri kujifunza kupiga mswaki na ikiwezena kutumia nyuzi za hariri (floss) kila siku
dr binafsi nashukuru kwa elimu ya maumivu ya tumbo ,lakini kwa upande wangu pia ningependa kusaidiwa ninahisi maumivu ya tumbo yapata miaka 2 ambayo huduma kwa siku kadhaa yakipotea hukaa kwa mda mrefu kidogo kisha hurejea tena na mara nyingine yanakuja kama vichomi kwenye mbavu, tumbo kujaa gesi na naweza kaa hata siku 4 sijapata choo.
Tutafute kwa namba zetu hapo, ninahitaji maelezo ya ziada kukusaidia
Asante na poleee sana
Nina maumivu ya tumbo yapata wiki Sasa. Tumbo linakoroga lakini siharishi na maumivu hasa chin ya kitovu
Pole sana
Maumivu ya tumbo sio jambo la ajabu kwa mtu yoyote, wakati mwingine tumbo linawza kuuma bila sababu yoyote ya msingi. Na huwa linaisha tu lenyewe
Ila likiendelea kwa muda mrefu inamaanisha kuna sababu, ni vzr kupima kinyesi ili kufahamu sababu
Kwa ajili ya kijisaidia unawza kumeza dawa za maumivu kama ibuprofen au paracetamol hzi zitapunguza maumivu ila hazitaondoa tatizo
Mwone daktar kama una maumivu ya tumbo na una homa
Namimi pia tangu jumapil napata maumivu ya tumbo na kuharisha then naona linanguruma sijui tatizo ni nini?
Namimi pia tangu jumapil napata maumivu ya tumbo na kuharisha then naona linanguruma sijui tatizo ni nini
pole sana ni vzr kumwona daktari akufannyie uchunguzi. pole sana