Mfumo wa chakula
Safari ya chakula ni ndefu na muhimu.
Umeng’enyaji wa chakula huanza pindi tu chakula kinapongia mdomoni na kutafunwa.
Mdomoni chakula hutafunywa na kutengeneza tonge moja linaloweza kumezeka.
Wakati wa kumeza chakula, ulimi hunyanyuka juu na kulielekeza tonge linapotoka kinywani.
Tonge hupita kwenye koo na baada kuingia kwenye umio.
Misuli ya umio inayokaza na kuachia hulisukuma tonge mpaka kufika tumboni
Misuli ya tumbo huendelea kukaza na kuchia ili kuvunja vunja chakula na kukichanganya na kemikali za umeng’enyaji zilizomo.
Chakula kilichomeng’enywa tumboni huvuka na kuelekea kwenye utumbo mdogo.
Vimeng’enya vilivyo kwenye utumbo mdogo huendelea kumeng’enya chakula kadri kinavyoshuka chini.
Ni kiasi kidogo tu cha virutubisho hufyonzwa chakula kinapokuwa tumboni
kiasi kikubwa cha ufyonzwaji wa virutubisho hufanyika kwenye utumbo mdogo.
Kuta za utumbo mdogo zimejaa viungo maalumu vinavyofanya kazi ya kufyonza virutubisho na kuvipeleka kwenye damu.
Kuna kiasi kidogo cha virutubisho vinavyoendelea kufyonzwa chakula kinapofikia utumbo mpana.
Kadri chakula kilichobakia bila kumeng’enywa kinapoendelea kupita kwenye utumbo mpana, kinaendelea kuwa kigumu na kutoka kama kinyesi.
Ni muhimu kulinda safari ya chakula mwilini.
- Kula mlo wenye nyuzinyuzi za kutosha
- Tafuna chakula vizuri
- Kunywa maji ya kutosha
- Fanya mazoezi
- Dhibiti msongo wa mawazo
- Acha kuvuta sigara
- Punguza kunywa pombe